MSANII WA MUZIKI WA KIZAZI KIPYA SAM WA UKWELI AFARIKI DUNIA



           MSANII WA MUZIKI WA KIZAZI KIPYA SAM WA UKWELI AFARIKI DUNIA



 
Msanii wa bongo flavor Salum Mohamed  aliyetamba kwa  jina la Sam wa ukweli amefariki dunia Usiku wa kuamkia 7,2018 Sam  alitamba  sana na kazi zake kama vile sina raha , alioutoa Mwaka 2010, usiniache loully , hata kwetu wapo
Baada ya ukimya wa muda mrefu alibuka tena   mwishoni mwa  2017,  na kibao kingine , kwa jina la kisiki, na  mwanzoni mwa   mwaka  2018, akauachia wimbo mwingine unaoitwa ni wewe
Ingawa ni mtu wa Singida Sam wa ukweli amekulia kiwangwa jirani na mji wa Dar es salaam  ambako amelelewa na Bibi yake mzaa Mama , kwa mujibu wa Meneja wake Abdulmalik Mohamed, mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hosipitali  ya Mwananyamala , jijini Dar es salaam , na mipango ya mazishi inaendelea katika eneo la Tandale, lakini maziko yatafanyika alhamisi hii kiwangwa mkoani Pwani
Na mwandishi, Tumaini Swai

Comments

Popular posts from this blog

PROFILE OF THE ARUSHA EAST AFRICAN TRAINING INSTITUTE

TAEATI