MKUU WA WILAYA YA ARUSHA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA BARABARA.



Mkuu wa  wilaya ya Arusha Mheshimiwa GABRIELI .F. DAQARO amefanya ziara yake  mkoani hapa ya kutembelea barabara ya TARURA  mijini na vijijini , ambayo imekuwa ikikarabatiwa kwanzia mwezi wa kwanza mpaka sasa na ametembelea barabara ya kata za kati, Levolosi , Terati na Murieti.
GABRIEL DAQARO, amesema kuwa wanatembelea kwasababu ni kazi yao ya  kawaida kutembelea miradi hiyo ili kujua kazi inayoendelea ndani ya wilaya na kazi inaenda vizuri lakini baadhi ya maeneo ni ya kusisitiza kwasababu kuna maeneo yanalegalega na wanatofautiana na mkataba waliyo pewa na serikali  katika utengenezaji wa barabara.
Ameendelea kwa kusema kwamba, kutokana na kampuni ambazo hazijafanya kazi kwa wakati muwafaka  amekubaliana na TARURA kwa kutaka kazi ziheshimiwe kulingana na mkataba uliowekwa na serikali na kufikia tarehe 14 mwezi wa nane mwaka huu 2019 kazi iwe imekamilika.
Hata hivyo amesema kuwa wapo wakandarasi ambao hawaeleweki na sababu wanazotoa ambazo siyo za msingi na wamesha toa maelekezo kwa TARURA kwa kuhakikisha kwamba wakandarasi ambao wanayumbayumba watambulike ili kwa kazi ya serikali ijayo watambulike ili kutokupewa kazi tena.
Vilevile Mheshimiwa mkuu wa wilaya amesema kuwa kila mwisho wa wiki wakandarasi na wasimamizi wote wanatakiwa kupeleka taarifa namna gani mradi huo unavyokwenda kwasababu wapo baadhi ya wakandarasi ambao hawapo site.
Aidha amesema kuwa wapo wakandarasi ambao hawalipi wafanyakazi  wanaofanya zile kazi za muda na ameelekeza TARURA wagunduwe stahiki za wafanyakazi hao walipwe shilingi elfu kumi (10000) kwa siku na  wahakikishe  kuwa watu hao hawanung’uniki,hawanyanyaswi na hawanyonywi.Na wahakikishe kwa wale wanaosuwasuwa  inapo bidi watavunja mkataba nao na waangalie thamani ya fedha.
Naye  kiongozi wa TARURA FODEM MWAKENJA amesema kuwa maelekezo haliotoa mkuu wa wilaya yatafanyiwa kazi kwa muda uliowekwa na serikali, na kwa wale wakandarasi ambao hawafati mikataba inasema nini watawachukulia hatua za kisheria .



Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe:GABRIELY.F.DAQARRO (katikati) akikagua miongozo ya kazi inayoendelea katika utengenezaji wa barabara ya TARURA mkoani Arusha. 

Comments

Popular posts from this blog

PROFILE OF THE ARUSHA EAST AFRICAN TRAINING INSTITUTE

TAEATI